IDARA YA ICT


Hii ni idara kati ya idara tisa (9) zilizopo katika casfeta mkoa wa Tanga. Idara hii hapo mwanzo haikuwepo, kuanzishwa kwa idara hii ya ict (Teknolojia, Habari na Mawasiliano) ilianza mwaka March, 2017 katika tawi la Casfeta Chuo Cha Ualimu Korogwe (TTC) tawi lililopo wilaya ya Korogwe mjini. Wazo la kuanzishwa kwa idara hii liliibuliwa na Mwenyekiti  wa tawi la Casfeta (TTC) Korogwe mjiini siku chache kabla ya kufanyika tamasha kubwa la kusifu na kuabudu lililofanyikia tawini hapo likihudhuliwa na watu toka makanisa mbalimbali na vikundi vingine vya kidini vilivyopo chuoni hapo. Idara hii ilianziahwa kwa lengo la kutunza taarifa kwa njia ya kielectronic zikiwemo taarifa za tawi, kuchapa barua kwa kutumia computer, kutengeneza matangazo mbalimbali, kurekodi na kuhifadhi matukio mbalimbali zikiwemo ibada na makusanyiko mengine.
Baada ya siku chache kiongozi huyo alichaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa Casfeta wilaya ya Korogwe pia akapendekeza kuwepo na idara hii ya ict kulingana na umhimu wake na faida ambayo iliyokuwa imeonekana kwa muda mfupi hapo tawini. Hivyo kwa madhumuni yale yale, liliongezwa wazo jingine la kufungua website pamoja na blog ya Casfeta wilaya ya korogwe. Mwenyekiti aliwachagua viongozi wa idara hii wenye utaalamu na masuala ya mitandao na computer programming wakiwemo mwenyekiti Lazaro Chingula, mwenyekiti msaidizi Erick John na Meshack Muna kama katibu wa idara.
Pia kwenye tamasha la pasaka mkoa wa Tanga lililofanyika mwezi wa nne mwaka 2017 wilayani korogwe, walichaguliwa viongozi wa casfeta mkoa wa Tanga ambapo Samwel Erasto alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa casfeta mkoa wa Tanga 2017/2018.
Mara baada ya kukabidhiwa majukumu alitangaza moja kwa moja kuanzishwa kwa idara ya ict mkoa wa Tanga. Aliwachagua na kutangaza viongozi wa idara hii ambapo aliwachagua na kuwatangaza viongozi wafuatao:-
Mwenyekiti – Lazaro Chingula
M/msaidizi – Erick John
Katibu – Meshack Muna
MAJUKUMU NA MALENGO MAKUU YA IDARA YA ICT
i)                    Kuwaunganisha wana – casfeta mkoa wa Tanga, walezi, wachungaji na wadau mbalimbali wa casfeta nje na ndani ya casfeta mkoa wa Tanga kwa njia ya mitandao.
ii)                   Kusambaza habari kwa njia ya mitandao. Zikiwemo matangazo ya mkoa, habari ya kielimu, taarifa za mitihani, matokeo kuanzia kidato cha kwanza hadi chuo.
iii)                 Kurekodi na kutunza kumbukumbu kwa njia ya kielectonic.
iv)                 Kutoa elimu kwa wana – casfeta na wadau mbalimbali juu ya faida na athari za mitandao na ukuaji wa teknolojia kwa kanisa la leo, hasa kwa vijana wa kizazi cha doti komu (kizazicha.com).
v)                  Kukuza na kuongeza kipato ndani ya casfeta mkoa wa Tanga na kuondoa au kupunguza hali ya utegemezi. (idara hii itatumika kama mradi wa kuingiza kipato ndani ya mfuko wa casfeta mkoa wa tanga).
vi)                 Kuwaimarisha wana – casfeta kiimani na hali ya kumtegemea Mungu kwa kuutunza wokovu pasipo mawaa kwa kupitia vipindi mbalimvbali vitakavyo endeshwa  mtandaoni na kuwafikia wana – casfeta popote walipo.
MBINU ZITAKAZO TUWEZESHA KUTIMIZA MALENGO
Nje na malengo ya kuanzisha casfeta Blog idara iliona mbali ikaamua pia kuanzisha CASFETA TV (Casfeta Online TV) ambayo itakuwa inarusha matangazo ya moja kwa moja yakiwemo makusanyiko ya Jointmass, December conference, mafundisho mbalimbali ya vijana yatakayo kuwa yanafundishwa na wachungaji mbalimbali pamoja na walezi wa casfeta mkoa na wilaya zake pia pamoja na makusanyiko mengine muhimu yakiwemo makusanyiko yanayofanyika makanisani pamoja na makusanyiko yanayohusu elimu kwani casfeta ni chombo kinachowaongoza wanafunzi waliopo mashuleni na vyuoni hivyo kuna ulazima na umuhimu wa kipekee wa kujua masuala ya kielimu.
Yakiwemo:-
·         Uchaguzi wa combination kulingana na taasusi ya kutaka kusomea hapo baadaye
·         Sifa za kujiunga na vyuo mbalimbali
·         Kupata matokeo mara baada ya kutangazwa na wizara husika yakiwemo matokeo ya darasa la saba, kidato cha nne, kidato cha sita pamoja na uchaguzi wa kujiunga na vyuo mbalimbali.
MAHITAJI YALIYOMO NDANI YA IDARA
Kama Casfeta Blog na Casfeta TV ni chombo kinachosimamiwa na idara ya ICT (Teknolojia, Habari na Mawasiliano) chini ya uongozi wa casfeta mkoa wa Tanga. Hivyo kama mdau unaweza kudonate kwenye blog yetu ili kusaidia huduma hii pamoja na ununuzi wa vifaa vifuatavyo.
·         Computer
·         Camera
·         Smartphone
·         Tablet
·         Empty DVD/CD
·        Pamoja na vifaa vingine vingi vya kielectronic vitakavyo tusaidia kuendesha Casfeta Blog na Casfeta TV mkoa wa Tanga.
UMILIKI WA CASFETA BLOG & CASFETA TV
Casfeta Blog & Casfeta TV Mkoa wa Tanga daima inamilikiwa na Casfeta Mkoa wa Tanga, ambapo Mwenyekiti ndiye kiongozi mkuu wa Casfeta Blog & Casfeta TV chini ya Mkurugenzi wa Casfeta Mkoa wa Tanga, wachungaji pamoja na walezi.
Kama ilivyo idara zingine mwenyekiti atahusika uteua na kuwatangaza viongozi ambao watakuwa wakiendesha Casfeta Blog & Casfeta TV kipindi chote cha uongozi wao.
Pia Mwenyekiti wa idara atawajibika kuchagua waendeshaji/watayalishaji wa vipindi mbalimbali vinavyorushwa na Casfeta Blog & Casfeta TV kutoka kila wilaya zilizomo mkoa wa Tanga.

0 comments:

Post a Comment

CASFETA VIDEOS

Followers

Chagua Mgawanyo wa habari

Total Page Views

Tuandikie Barua Pepe

Name

Email *

Message *